Msanii wa filamu, Steve Nyerere amesema Wema Sepetu alikuwa hajitoi kwenye matatazo ya wasanii wenzake wa filamu na ndio maana wasanii wengi wa filamu wakashindwa kuhudhuria katika mazishi ya baba yake, Balozi Isaac Abraham Sepetu mwishoni mwa mwezi uliopita.
Akizungumza leo Steve,amesema anawataka watu waache kumtupia lawama Vicent Kigosi aka ‘Ray’ wakati mwanadada huyo alikuwa hahudhurii katika matatizo ya wenzake.
“Mnamlaumu bure Ray jambo ambalo hajafanya kwakuwa Ray ni jalala basi kila kitu mnamtupia,jamani mwacheni apumzike,” amesema Steve.
“Sisi katika Bongo Movie Unity tuna uongozi, tuna mwenyekiti,tuna mwenyekiti wa mipango ambaye ndio mimi, na tuna makamu wa mwenyekiti ambaye ndio mimi na tuna makamu mwenyekiti ambaye ni Irene Uwoya. Lakini sisi taratibu zetu kwenye misiba kama unaona kwenye misiba yetu tunajitoa,lakini linavyotufika tunaangalia ni mwanachama gani naye anakua anajitoa katika misiba ya wenzake
Pesapal Yaja na suluhisho la kisasa kusimamia uendeshaji wa vituo vya mafuta
Mfanyakazi was Lake oil akimgudumia mteja.kampuni ya Pesapal imezindua suluhisho inayowawezesha wamiliki wa vituo vya mafuta kuweza kufuatilia na kusimamia...
Read more