Wadau wa muziki wa Bongo Fleva tuliisubiri kwa hamu kubwa video ya wimbo wa mkongwe wa muziki nchini Tanzania, Joseph Haule maarufu kama Prof. Jay.
Siku ya leo Prof. Jay ameachia rasmi video ya wimbo huo unaojulikana kama “Kipi Sijasikia” akiwa amemshirikisha mkali Diamond Platnumz. Video hiyo ina mandhari mbalimbali ikiwemo mahakamani, na sehemu za starehe na pia imebeba watu wenye majina makubwa Tanzania akiwemo prodyuza mkongwe nchini na ambaye ametengeneza audio ya Kipi sijasikia, P Funck Majani. Muigizaji maarufu kama Dude, na mastaa wengine wengi akiwemo Dj Choka pia wameng’arisha video hiyo. Ili kupata uhondo zaidi nimeitupia hapa video hiyo ili uweze kushuhudia kwa macho yako mwenyewe:
NMB, Oryx Tanzania wazindua ‘Moto Mkali Bei Poa,’ kukopesha gesi ya kupikia
NA MWANDISHI WETU BENKI ya NMB imeingia Makubaliano ya Ushirikiano (MoU) na Kampuni ya Uuzaji na Usambazaji Gesi ya Oryx...
Read more