
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mhe. Innocent Bashungwa ameonesha kutoridhishwa na kasi na viwango vya ujenzi wa Kituo cha Afya Kibona.
Kutokana na hali hiyo, ametoa miezi miwili kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe kuhakikisha anasimamia ukamilishaji wa Kituo cha Afya Kibona ili kianze kutoa huduma kwa wananchi.
Waziri Bashungwa ameyasema hayo Julai 18, 2022 wakati wa kukagua ujenzi wa Kituo cha Afya Kibona kilichopo kata ya Kanoni Wilaya Karagwe.
SOURCE: TAMISEMI_Facebook