Uongozi wa klabu ya Yanga umetoa onyo kwa wale wanaojihusisha na utengenezaji na uuzaji wa jezi feki ambazo hutumia nembo (logo) ya klabu hio kuzifanya zionekane kama ni Jezi original kama zinazozalishwa na mzabuni mwenye dhamana ya kuzalisha na kusambaza jezi hizo ambayo ni kampuni ya GSM. Hivyo kwa mujibu wa Uongozi wa klabu hio imewakumbusha tu kuwa ni kosa kisheria kutumia nembo hio katika jezi feki, ni kampuni ya GSM pekee ndio mzabuni wa kutengeneza jezi hizo.
MO DEWJI AIWAKIA VUNJABEI KUONDOSHA MATANGAZO YA MO JEZI MPYA
Mkurugenzi wa Makampuni ya METL Group na Mwekezaji wa klabu ya Simba, Mohammed Dewji MO kupitia ukurasa wa Twitter wa...
Read more