
Infantino mwenye umri wa miaka 52, amepita bila ya kupingwa kwenye kongamano lililofanyika Kigali nchini Rwanda leo siku ya Alhamisi.
Mwanasheria huyo ameiongoza FIFA tangu kuondoka kwa utawala wa Joseph Blatter, mnamo mwaka 2016 na bado anayo nafasi ya kuwania tena mwaka 2027.
“Kuwa Rais wa FIFA ni heshima kubwa, ninashukuru na kuguswa na sapoti yenu. Nitaendelea kuhudumu FIFA, nitautumikia mpira dunia nzima, nitahudumia mashirikisho yote 211 ya FIFA”, amesema, Infantino.
–
Lakini nchi kadhaa za Ulaya, zikiwemo Ujerumani, Norway na Sweden, hazijafurahishwa na urais wake na zimesema hazitamuunga mkono kikamilifu.