Chelsea wanataka kitita cha pauni milioni 70 kumuuza kiungo wa kati wa England Mason Mount, 24, licha ya kusalia na mwaka mmoja wa mwisho wa kandarasi yake. (Athletic)
Mount ana nia ya kujiunga na Bayern Munich na kuungana na meneja wake wa zamani wa Chelsea Thomas Tuchel. (Guardian)
Mabingwa wa Ujerumani Bayern Munich wanakaribia kukamilisha dili la kocha msaidizi wa Chelsea Muingereza Anthony Barry. (90Min)
Lakini kiungo wa kati wa West Ham Declan Rice, 24, hasakwi na Bayern na hawakufanya mkutano na wawakilishi wa mchezaji huyo wa kimataifa wa England wiki iliyopita. (Sky Sports Ujerumani)