Naibu Waziri Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Dkt. Festo J. Dugange(Mb) amesema Serikali katika mwaka wa fedha 2022/23 imetenga shilingi bilioni 35.1 kwa ajili ya ununuzi wa magari 316 ya kubebea wagonjwa katika vituo vya kutolea huduma za afya nchini.
Amesema hayo leo tarehe 24 Aprili 2023 Bungeni Dodoma wakati akijibu Swali la Mbunge wa Jimbo la Mfindi Kusini, Mhe. David Mwakiposa Kihenzile aliyetaka kujua Je, ni lini Serikali itapeleka magari ya kubebea Wagonjwa katika Vituo vya Afya vya Mtwango na Mgololo.